Header Ads

test

HISTORIA YA KANISA NA Mwl. N Chaligha

HISTORIA YA KANISA NA UKRISTO WETU!!!
    Hapo mwanzo wanafunzi wa Yesu hawakujulikana kwa Jina la "WAKRISTO"
Kwa mara ya kwanza waliitwa,"WAKRISTO" huko Antiokia. Matendo 11:26
Baada ya Bwana Yesu kufa,kufufuka na kupaa,wanafunzi walienda huko na huko(ulimwenguni kote ) kuhubiri injili.
Baada ya mafanikio ya mwanzo ya Injili yaliyopelekea maelfu ya watu kuongoka,wanafunzi walifanya kosa la kuanzisha Kijiji cha ujamaa. Badala ya kulipeleka jeshi kwenye kazi ya injili.,walifanya kazi ya kumega mkate nyumba kwa nyumba. Matendo2:44-47
Hii ilipelekea jeshi la adui,kuingia ndani ya kanisa na kuleta choyo,ubinafsi,ulafi ,magomvi na manung'uniko. Matendo 6:1
Kanisa la Mungu,mahali popote na wakati wowote linapoacha huduma ya Injili kwa wadhambi na kubaki kujitazama lenyewe(tule nini,tunywe nini,tuanzishe miradi gani,tujiimarisheje kifedha)basi Kanisa hilo litegemee magomvi yasiyoisha Kati yao. Hata mbwa asiyefundishwa kuwinda huwa mwizi wa mayai.
Ili litimie kusudi la Mungu la kuhubiri injili kwa kila kiumbe,Mungu alikivunja Kijiji chao Kwa kuruhusu mateso kwao baada ya kifo cha Stefano.Tunasoma kuwa Sauli(Paulo )akaliharibu kanisa,akiingia nyumba kwa nyumba na kuwaburuta wanaume na wanawake na kuwatia gerezani.Matendo8:1-3
Hii ilisaidia sana kuenea kwa injili,kwani iliwapelekea watu wote kutawanyika na kwenda huko na huko wakihubiri neno.Matendo8:4
Ndipo Mungu akaongeza nguvu kwenye jeshi la Bwana kwa kumwongoa Sauli(Paulo )
Ashukuriwe, Mungu kwani mtu huyu Kwa ujasiri wake UKRISTO ulienea kwa kasi kwenye nchi za kipagani(Rumi,n.k.)



 HISTORIA YA KANISA NA UKRISTO WETU (2)
    Katika maelezo yangu ya kwanza,nilieleza kidogo kuwa Mungu alimwingiza Paulo katika huduma ya Injili.
Mitume walienda huko na   huko hadi Asia ndogo,India, Ethiopia hadi Afrika Kaskazini.Petro na Paulo walihubiri huko Rumi(Italia)

UKRISTO HUKO RUMI:
     Wakristo wa Kanisa la Karne ya 1-3 walipata mateso makali sana. Waliteswa sana na wapagani wa wakati huo.Na haya mateso hapo Rumi yalikuwa makali sana.Mtawala mmoja aitwaye Nero alijulikana kwa ukatili wake. Ndiye aliyemwua Petro.Wakristo walitupwa katikati ya simba wengi wenye njaa ili waliwe. Wengine walitupwa kwenye matanuru ya moto wakiwa hai.Wengine walisulubishwa(Petro) na wengine waliuwawa kwa kukatwa vichwa(Paulo)
Kuwa Mkristo na kuhubiri Kwa wakati ule kulimaanisha mateso na kifo.
Njia ya Yesu ni njia ya dhiki na mateso tangu mwanzo wake hadi mwisho wake.Matendo14:22 .Mimi naamini kipimo cha Mkristo mwaminifu ,ni dhiki udhia,mateso,vifungo,kukataliwa,kutengwa na masinagogi. Vizazi vyote,na hata sasa watu waaminifu wamelipia gharama ya ukristo wao(mateso).Hata mwandishi wa makala hii amewahi kulipia gharama hii.Amefungwa gerezani Mwaka mmoja kwa ajili ya Yesu(1978) Amewahi kufukuzwa mara 3 akihubiri injili. Mara moja alifukuzwa Kwa mawe.Mwaka 1992 alipona kupigwa risasi huko Mbozi(Mbeya)wakati akihubiri Injili,ikamlazimu kutembea usiku kucha bila viatu kwenye barabara ya kokoto. Amewahi kutengwa na sinagogi,na kunenwa vibaya mara nyingi kwa ajili ya Injili.
Najua kuwa sijafikia kipimo cha mateso ya Baba zangu wa Imani.Lakini naamini nami yapo machozi ya kufutwa ktk. siku Ile (japokuwa ni machache)
NAKAZA MWENDOOOO!!!!!!!!
        MAPAPA(POPES)
       Rumi ya kipagani iliwatesa Wakristo hadi Karne ya 3. Kwenye Karne ya 4 aliongoka mtawala wa kirumi aitwayeConstantine.Kuongoka kwake kulipelekea Kanisa kupumua kidogo mateso. Kukoma Kwa mateso kulipelekea Kanisa kupokea waongofu wengi,Ila waongofu nusunusu. Shetani akaitumia tena nafasi hii kuingiza uharibifu ndani ya kanisa.
Labda kabla sijaendelea mbele nieleze kidogo juu ya kanisa la Roma na uongozi wa PAPA(POPE).
Jina Papa ,maana yake ni "BABA" Lina asili ya kigiriki,"PAPA"
     

No comments:

Powered by Blogger.